NA ALBERT G. SENGO/ ARUSHA
Napata fursa ya kutembelea Makumbusho ya Azimio la Arusha yaliyoko eneo la Kaloleni, karibu na Mnara wa Uhuru (Mnara wa Mwenge). Hadi mwaka 1967, jengo hili lilitumika kama ukumbi wa ustawi wa jamii kwa jamii ya Kaloleni jijini Arusha. Mnamo Januari 1967, jengo hilo lilikuwa na mkutano wa kihistoria ambao Sera ya Kisiasa na Kiuchumi ya Tanzania ya Ujamaa na Kujitegemea ilitolewa. Mnamo Februari 1977 jengo hilo lilibadilishwa kuwa jumba la kumbukumbu ndogo la kisiasa na uchumi. Jeh ni yapi yaliyomo ndani ya Makumbusho haya? Ungana nami msimulizi wako Albert G. Sengo nikupitishe hatua kwa hatua katika eneo hili ambalo ni nyenzo muhimu ya kufundishia kwa historia, kiraia, masomo ya jumla na masomo ya sayansi ya siasa.Tuesday, April 30, 2024
ZEE LA NYETI AJILAUMU KIFO CHA GADNA - "UKISIKIA MTU ANAUMWA USIAHIRISHE NENDA KAMSABAHI"
NA ALBERT G. SENGO/ ROMBO, KILIMANJARO
Mwandishi wa Habari za Burudani na Michezo wa Gazeti la Mwananchi ambaye pia ni Mtangazaji na Mjasiliamali, Henry Mdimu 'Zee la Nyeti' amezungumza na Jembe Fm wakati wa mazishi ya mwanahabari nguli wa Clouds Fm, Gadna G. Habash, jinsi alivyoguswa na msiba wa marehemu huyo aliyefariki asubuhi ya Jumamosi ya tarehe 20 April 2024 baada ya kuugua na kulazwa katika Hospitali ya Jakaya Kikwete jijini Dar es salaam. Mdimu ameiasa jamii kutopuuzia suala la kwenda kwa wakati kuwajulia hali wapendwa wao wanapougua kwani yeye aliahirisha mara kadhaa kwenda kumtembelea hospitalini marehemu Gadna wakati alipopata taarifa za kulazwa kwake. "Nimejuta Gadna wiki moja kabla ya kifo chake nilikuwa nafanya show Morogoro kwahiyo tuklikuwa tumeshaelewana, tumeshalipana hela ya tangazo lakini kesho yake nikasikia jamaa amelazwa, nikawaambia stuff wangu msimsumbue huyu jamaa kwasababu nimetoka naye mbali, tutakuja kufanya naye tangazo siku nyingine na nikirudi Dae es salaam nitakuja kumwona" "Nimeenda Dar es salaam nimekaa siku tatu, sikupata nafasi ya kwenda hospitali lakini nilikuwa napiga simu kwa marafiki, jamani kuna mtu amekwenda kumwona Gadna?'" Jibu - "Yes" Swali - "Anaendeleaje?" Jibu - "Yuko Powa" "Basi nikasema niende tena Morogoro nikirudi nitamkuta, nafika tu Morogoro nasikia Gadna amefariki"............ #samiasuluhuhassan #mwanza #rombo #gadnaMKE WA MBUNGE JIMBO LA KIBAHA MJI ATIMIZA AHADI YAKE KWA VITENDO VIJANA WA HAMASA
NA VICTOR MASANGU KIBAHA
MWENGE WA UHURU WATOA BARAKA KWA RUWASA MRADI WA MAJI FUKAYOSI UENDELEE
NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO
Wananchi wapatao elfu 3666 katika kijiji cha Kidomole pamoja na vitongoji vyake mbali mbali vilivyopo katika kata ya Fukayosi Wilayani Bgamoyo Mkoa wa Pwani wanatarajia kuondokana na changamoto ya usumbufu wa majii fikapo mwezi Mei mwaka huu baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji ambao utakuwa ni mkomboz mkubwa kwa wananchi hao.
Hayo yamebainishwa na Meneja wa wakala wa Usambazaji wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Wilaya ya Bagamoyo James kionaumela wakati akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa ndugu Godfrey Mnzava kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo ambapo alisema kwa sasa upo katika hatua za mwisho kwa ajili ya upanuzi.
Meneja huyo alibainisha kwamba unatekelzwa chini ya mkandarasi mzawa AM&Partiner Limeted na Building Contractors kutoka jijini Dar es Salaam na kwamba kwa mujibu wa mkataba huo mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Mei 11 mwaka huu.
Alifafanua kwamba katika upanuzi wa mradi huo pia unakwenda sambamba na ujenzi wa tibio la maji katika eneo la Saadan na kwamba mradi huo umegharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 603 ambazo ni fedha kutoka katika mfuko wa maji( NWF)
Meneja huyo alibainiha kwamba utekelezaji wa mradi huo ulianza rasmi mnamo tangu Mei 11 mwaka 2023 na pia utaweza kuzinufaisha kaya zipatazo 796 kutoka kata ya Fykayosi pamoja na vitongoji vyake wananchi wataweza kuondokana na changamoto ya maji na hatimaye kupata huduma ya maji safi na salama.
Pia alisema kuwa katika kutekeleza mradi huo umeweza kutoa fursa mbali mbali za ajira kwa vijana wa lika mbali mbali wapatao 50 ambao kwa sasa wameweza kujipatia kipato halali na kujikwamua kiuchumi.
Meneja huyo alibainisha kwamba katika eneo la kijiji cha Kidomole utekelezaji wa mradi huo umefikia kwa kiwango cha asilimia 90% ikiwa ni pamoja na ujenzi wa tanki kubwa lenye ujazo wa lita elfu 50,000 kwenye mnara wa mita 12.
Katika hatua nyingine Meneja huyo alitoa shukrani za dhati kwa Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anatenga fedha katika kuboresha sekta ya maji kwa vitendo lengo ikiwa ni kuwapatia huduma wananchi ya maji safi na salama.
Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Godfrey Mnzava pamoja na wakimbiza mwenge wenzake wameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kukubaliana kwa pamoja kuupitisha pamoja na kuwapongeza Ruwasa kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya katika kuwapelekea huduma ya maji wananchi.
Alisema kwamba huduma ya maji ni muhimu sana kwa wananchi hivyo Ruwasa waendelee kuchapa kazi kwa bidii na kuhakikisha wanatekeleza miradi ya maji kwa kiwango ambacho kinastahili kulingana na fedha ambazo zinatolewa na Rais.
Monday, April 29, 2024
MIRADI YA TRILIONI 8.5 KUTEMBELEWA NA MWENGE WA UHURU MKOA WA PWANI.
VICTOR MASANGU,CHALINZE
Saturday, April 27, 2024
DOZI MOJA INATOSHA KUFANIKISHA KUZUIA SARATANI SHINGO YA KIZAZI.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu. |
NI maadhimisho ya ‘dozi ya chanjo ya HPV’, inayomkinga mtoto wa kike asipate ugonjwa wa saratani ya mlango wa shingo ya uzazi.
Chanjo hiyo ya HPV inawalenga watoto wenye umri kati ya miaka tisa na 14, ambayo Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, anasema kuwa dozi moja inatosha kumkinga msichana kupata ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.
Waziri Ummy anayaongea hayo kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Dozi moja ya chanjo ya HPV kwa wasichana, akinena ni jukumu la wazazi na walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto kupata chanjo hiyo.
Ni hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Furahisha Wilayani Ilemela, Mwanza akiwa na ufafanuzi: “Wataalamu wetu ambao wanatoka kwenye Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR).
“Wametuhakikishia kuwa dozi moja ya chanjo ya HPV inatosha kumkinga msichana kupata saratani ya mlango wa kizazi.”
Anasema awali dozi zilitolewa mbili, ya pili ikiwa ni miezi sita akipelekewa binti, hata hivyo wengi hawakurudi kumalizia.
Lakini anaeleza mbadala uliopo ni kwamba, hivi sasa anasema wanatoa dozi moja, inayotosha kuwakinga wasichana dhidi ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi.
Waziri anaeleza saratani inayoongoza kuwatesa Watanzania ni ‘Mlango wa Kizazi’ anayosema katika kila wagonjwa100, wako 23 wagonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.
Anaorodhesha saratani zinazofuatia kwa ukubwa ni inayohusu: Mfumo wa Chakula, asilimia 11; matiti asilimia 10.4; tezi dume asilimia 8.9.
Pia, Waziri anatoa wito kwa wazazi na walezi nchini, kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo zote wanazopaswa, ili wanufaike na kinga dhidi ya maradhi yaliyotajwa, ikiwamo lengo kubwa la kuwakinga na magonjwa, yakiwamo haya ya saratani pamoja na kuwakinga na vifo vinavyoweza kuzuilika na chanjo.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi. |
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza, Saidi Mtanda atahakikisha watoto wote wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi 14, wanapata chanjo hiyo ili kufikia malengo.
“Kwa mwaka 2022/23 Mkoa wa Mwanza ulifanikiwa kuchanja watoto zaidi ya laki Mbili sawa na asilimia 107 kati ya walengwa waliotarajiwa kuchanjwa ni laki 191,440 wenye umri chini ya mwaka mmoja, tumefikia malengo na kuyavuka,” anasema.
Mkazi wa Jiji la Mwanza Amina Said, anasema kutolewa kwa chanjo hiyo ni moja ya mapambano ya kumkinga mtoto wa kike asipate saratani ya mlango wa kizazi.
Anasema elimu juu ya chanjo hiyo inatakiwa kutolewa mara kwa mara ili jamii iendelee kuelewa umuhimu wa chanjo hiyo.
"Mimi nina mtoto wa kike ana umri wa miaka name,lakini sina elimu yoyote, kuwa anapofikisha miaka tisa anatakiwa kupatiwa chanjo hiyo," anasema.
Anaongeza kuwa, serikali inapambana kuwahakikishia wananchi wake wawe na afya njema, hivyo ana rai elimu iendelee kutolewa kwa jamii, ijue umuhimu wa chanjo.
Aziza Jumanne, mkazi wa Mwanza anaitaja chanjo hiyo kuwa mkombozi kwa wasichana wenye sifa ya kupata chanjo hiyo, akiishauri jamii izingatie jinsi ya kuwasaidia watoto wa kike wasipate ugonjwa huo.
"Kila mzazi ambaye ana mtoto wa kike aliye na sifa za kupata chanjo, awapeleke kupata chanjo hiyo," anasema, kuwa watoto wanapopatiwa chanjo, wananudhurika kwa maradhi hayo.
Anthony Andrew, mkazi wa Maduka Tisa, jijini Mwanza anasema ni wakati wa wazazi na walezi kuachana na mila potofu dhidi ya kuwapo chanjo hizo na kinachotakiwa ni kuisaidia serikali, ili watoto wapate waelewe.
Andrew anakumbusha chanjo inatolewa bure na inabaki jukumu la walezi na wazazi kujitokeza na watoto wao waweze kupatiwa chanjo hiyo.
"Tumekuwa tunasikia kutoka kwa wataalamu wetu wa afya, magonjwa sugu yanayo changia vifo kwa jamii. Katika magonjwa hayo, saratani nayo ipo," anasema, akiwa na ufafanuzi.
Anaongeza kuwa, saratani zote zina changamoto zake, kama mtu atachelewa kupata matibabu kwa wakati anayonafasi kubwa ya kupoteza maisha.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya waandishi wa habari wakichukuwa matukio na taarifa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, viwanja vya Furahisha Mwanza.
Binti aliyetia fora katika uwasilishaji wa shairi lenye kutia hamasa kwa wazazi kushiriki vyema kuhakikisha watoto wanapatiwa chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi, wakiwa katika Uzinduzi wa maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Kutoka Bujora ni kundi la ngoma likinogesha shughuli katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Wednesday, April 24, 2024
MSIFANYE KAMPENI KINYEMELA KABLA YA MUDA WAKE -KATIBU CCM KIBAHA MJI
NA VICTOR MASANGU,KIBAHA
Saturday, April 20, 2024
LEO BARABARA ZOTE ZA JIJI LA DAR ES SA;AAM KUELEKEA MWENGE - TANGAZO ANOINTED MINISTRY 2024
𝗘𝘄𝗲 𝗺𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗠𝘂𝗻𝗴𝘂 𝗵𝗶𝗶 𝗶𝗻𝗮𝗸𝘂𝗵𝘂𝘀𝘂 𝗻𝗶 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝘁𝗮𝗿𝗲𝗵𝗲 𝟮𝟬𝘁𝗵 𝗔𝗽𝗿𝗶𝗹 𝟮𝟬𝟮𝟰 𝗗𝗮𝗿 𝗲𝘀 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺 𝗶𝘁𝗮𝘁𝗶𝗸𝗶𝘀𝗶𝗸𝗮....
. . . . . #JEMBEGOSPLEJESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI PWANI LAWAFUNDA WANANCHI JUU YA KUJIKINGA NA MAFURIKO NA MAAFA
Friday, April 19, 2024
RFO PWANI-TUMEFANIKIWA KUOKOA WANANCHI 2397 MAFURIKO YA RUFIJI NA KIBITI
NA VICTOR MASANGU,PWANI
WAZIRI JERRY SILAA KUONGOZA KLINIKI YA ARDHI TANGA
WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.
Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.
Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.
“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema
Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.
Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani
Thursday, April 18, 2024
RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA ALAT 2024 UTAKAOFANYIKA ZANZIBAR
𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 mgeni rasmi Mkutano wa 38 ALAT utakaofanyika Tarehe 23 - 25 April 2024 #Zanzibar
. . #alat @ortamisemi @samia_suluhu_hassan @dr.hmwinyi @jembenijembe @kikotifredy #samiasuluhuhassan #HUSSEINMWINYI #zanzibar