ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 30, 2024

'HAYA NDIYO NILIYOYAKUTA NDANI YA HIFADHI YA MAKUMBUSHO YA AZIMIO YA ARUSHA'

 NA ALBERT G. SENGO/ ARUSHA

Napata fursa ya kutembelea Makumbusho ya Azimio la Arusha yaliyoko eneo la Kaloleni, karibu na Mnara wa Uhuru (Mnara wa Mwenge). Hadi mwaka 1967, jengo hili lilitumika kama ukumbi wa ustawi wa jamii kwa jamii ya Kaloleni jijini Arusha. Mnamo Januari 1967, jengo hilo lilikuwa na mkutano wa kihistoria ambao Sera ya Kisiasa na Kiuchumi ya Tanzania ya Ujamaa na Kujitegemea ilitolewa. Mnamo Februari 1977 jengo hilo lilibadilishwa kuwa jumba la kumbukumbu ndogo la kisiasa na uchumi. Jeh ni yapi yaliyomo ndani ya Makumbusho haya? Ungana nami msimulizi wako Albert G. Sengo nikupitishe hatua kwa hatua katika eneo hili ambalo ni nyenzo muhimu ya kufundishia kwa historia, kiraia, masomo ya jumla na masomo ya sayansi ya siasa.

ZEE LA NYETI AJILAUMU KIFO CHA GADNA - "UKISIKIA MTU ANAUMWA USIAHIRISHE NENDA KAMSABAHI"

 NA ALBERT G. SENGO/ ROMBO, KILIMANJARO

Mwandishi wa Habari za Burudani na Michezo wa Gazeti la Mwananchi ambaye pia ni Mtangazaji na Mjasiliamali, Henry Mdimu 'Zee la Nyeti' amezungumza na Jembe Fm wakati wa mazishi ya mwanahabari nguli wa Clouds Fm, Gadna G. Habash, jinsi alivyoguswa na msiba wa marehemu huyo aliyefariki asubuhi ya Jumamosi ya tarehe 20 April 2024 baada ya kuugua na kulazwa katika Hospitali ya Jakaya Kikwete jijini Dar es salaam. Mdimu ameiasa jamii kutopuuzia suala la kwenda kwa wakati kuwajulia hali wapendwa wao wanapougua kwani yeye aliahirisha mara kadhaa kwenda kumtembelea hospitalini marehemu Gadna wakati alipopata taarifa za kulazwa kwake. "Nimejuta Gadna wiki moja kabla ya kifo chake nilikuwa nafanya show Morogoro kwahiyo tuklikuwa tumeshaelewana, tumeshalipana hela ya tangazo lakini kesho yake nikasikia jamaa amelazwa, nikawaambia stuff wangu msimsumbue huyu jamaa kwasababu nimetoka naye mbali, tutakuja kufanya naye tangazo siku nyingine na nikirudi Dae es salaam nitakuja kumwona" "Nimeenda Dar es salaam nimekaa siku tatu, sikupata nafasi ya kwenda hospitali lakini nilikuwa napiga simu kwa marafiki, jamani kuna mtu amekwenda kumwona Gadna?'" Jibu - "Yes" Swali - "Anaendeleaje?" Jibu - "Yuko Powa" "Basi nikasema niende tena Morogoro nikirudi nitamkuta, nafika tu Morogoro nasikia Gadna amefariki"............ #samiasuluhuhassan #mwanza #rombo #gadna

MKE WA MBUNGE JIMBO LA KIBAHA MJI ATIMIZA AHADI YAKE KWA VITENDO VIJANA WA HAMASA

 


NA VICTOR MASANGU KIBAHA 


Jumuiya ya Umoja wa vijana ya Chama cha mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kibaha mji umempongeza kwa dhati mke wa Mbunge wa  Jimbo la Kibaha mji Selina Koka kwa kuona umuhimu wa kuwasapoti vijana kwa kutoa  msaada wa  mahitaji na vitu  mbali mbali ikiwa ni utekelezaji wa ahadi zake alizozitoa  kwa vijana.


Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kibaha mjini Gamalu Makona wakati wa halfa fupi ya kukabidhiwa baadhi ya mahitaji na vitu mbali mbali kwa ajili ya kuwasaidia vijana wa hamasa ambao wapo katika mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na  kuupokea Mwenge wa uhuru.
Aidha Katibu huyo alisema kwamba Mama Koka amekuwa mstari wa mbele katika kusaidia mambo mbali mbali katika jumuiya ya vijana katika Jimbo la Kibaha mji.

Aliongeza kwamba Mama Koka amewashika mkono na kuwapatia msaada wa vyakula mbali mbali,sambamba na mabati viti meza kwa ajili ya ujenzi wa banda ambalo litakuwa linatumika kukutana vijana wa uvccm pamoja na kupumzikia ili kujadili mambo ya jumuiya na maendeleo.

"Kwa kweli tunamshukuru na kumpongeza Mama Koka kwa kuwa na upendo wa kipekee maana hivi karibuni alikuja kututembelea umoja wetu na kile ambacho alituahidi kiukweli amekitekeleza na Mungu aweze kumbariki yeye pamoja na Mbunge kwa kuwa na moyo wa kujitolea,"alisema Katibu.

Akikabidhi msaada huo wa vitu mbali mbali kwa niaba ya Mama Koka Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Method Mselewa alisema kwamba msaada huo ni moja ya utekelezaji wa ahadi ya mke wa Mbunge kwa vijana hao ambayo aliitoa alipokwenda kuwatembelea hivi karibu.

Katibu Method alisema Mama Koka anatambua mchango mkubwa ambao unafanywa na jumuiya ya vijana hivyo akaamua kutoa mahitaji mbali mbali ambayo yatawasaidia vijana pindi wanapokuwa wakiendelea na mazoezi yao ya kujiandaa na Mwenge wa uhuru.

Mselewa alibainisha kwamba vijana hao ni Taifa la kesho hivyo wanapaswa kupendana na kuwa na maadili mazuri pamoja na  uzalendo kwani ndio viongozi watarajiwa katika siku za usoni.

"Hapa nimekuja kwa niaba na mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Koka na nimekuja na vitu mbambali kwa ajili ya chakula pamoja na redio ambayo mtakuwa mkiitumia katika burudani na mambo mengine,"alifafanua Katibu huyo.

Aliwahimiza vijana kuendelea kufanya mazoezi pamoja na kushiriki kikamilifu katika kuupokea Mwenge wa uhuru ambao utatembelea miradi mbali mbali ya maendeleo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon ambaye naye alifika kuwajulia hali vijana hao wa hamasa amewahimza kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika ujio wa mapokezi ya mbio za Mwenge wa uhuru na kwamba serikali ipo pamoja nao.

Katika hatua nyingine aliwaahidi katika mkesha wa mwenge kutakuwa na burudani mbali mbali za wasanii wakubwa pamoja na wasani wa kibaha na kwamba siku hiyo wategemee kuona burudani ya aina yake hivyo wajitokeze kwa wingi.

MWENGE WA UHURU WATOA BARAKA KWA RUWASA MRADI WA MAJI FUKAYOSI UENDELEE

 


NA VICTOR MASANGU, BAGAMOYO


Wananchi wapatao elfu 3666 katika kijiji cha Kidomole  pamoja na vitongoji vyake mbali mbali vilivyopo katika  kata ya Fukayosi  Wilayani Bgamoyo Mkoa wa Pwani wanatarajia kuondokana na changamoto ya usumbufu wa majii fikapo mwezi Mei mwaka huu baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji ambao utakuwa ni mkomboz mkubwa kwa wananchi hao.

Hayo yamebainishwa na  Meneja wa wakala wa Usambazaji wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Wilaya ya Bagamoyo  James kionaumela wakati akitoa taarifa kwa kiongozi wa mbio za Mwenge  wa Uhuru  kitaifa ndugu  Godfrey Mnzava kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo ambapo alisema kwa sasa upo katika hatua za mwisho kwa ajili ya upanuzi.


Meneja huyo alibainisha kwamba unatekelzwa chini ya mkandarasi mzawa AM&Partiner Limeted na Building Contractors kutoka jijini Dar es Salaam na kwamba kwa mujibu wa mkataba huo mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Mei 11 mwaka huu.

Alifafanua kwamba katika upanuzi wa mradi huo pia unakwenda sambamba na ujenzi wa  tibio la maji katika eneo la Saadan na kwamba mradi huo umegharimu kiasi cha   zaidi ya  shilingi milioni 603 ambazo ni fedha kutoka katika mfuko wa maji( NWF)





Meneja huyo alibainiha kwamba utekelezaji wa mradi huo ulianza rasmi mnamo tangu Mei 11 mwaka 2023 na pia utaweza kuzinufaisha kaya zipatazo 796 kutoka kata ya Fykayosi pamoja na vitongoji vyake wananchi wataweza kuondokana na changamoto ya maji na hatimaye kupata huduma ya maji safi na salama.

Pia alisema kuwa katika kutekeleza mradi huo umeweza kutoa fursa mbali mbali za ajira kwa vijana wa lika mbali mbali  wapatao 50 ambao kwa sasa wameweza kujipatia kipato halali na kujikwamua kiuchumi.

Meneja huyo alibainisha kwamba katika eneo la kijiji cha Kidomole utekelezaji wa mradi huo umefikia kwa kiwango cha asilimia 90% ikiwa ni pamoja na ujenzi wa tanki kubwa lenye ujazo wa lita elfu 50,000 kwenye mnara wa mita 12.

Katika hatua nyingine Meneja huyo alitoa shukrani za dhati kwa Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anatenga fedha katika kuboresha sekta ya maji kwa vitendo lengo ikiwa ni kuwapatia huduma wananchi ya maji safi na salama.

Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Godfrey Mnzava pamoja na wakimbiza mwenge wenzake wameridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kukubaliana kwa pamoja kuupitisha pamoja na kuwapongeza Ruwasa kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya katika kuwapelekea huduma ya maji wananchi.

Alisema kwamba huduma ya maji ni muhimu sana kwa wananchi hivyo Ruwasa waendelee kuchapa kazi kwa bidii na kuhakikisha wanatekeleza miradi ya maji kwa kiwango ambacho kinastahili kulingana na fedha ambazo zinatolewa na Rais.

Monday, April 29, 2024

MIRADI YA TRILIONI 8.5 KUTEMBELEWA NA MWENGE WA UHURU MKOA WA PWANI.

 

VICTOR MASANGU,CHALINZE


Mbio za Mwenge wa Uhuru umewasili leo rasmi mkoani Pwani ukitokea Mkoani Morogoro ambapo umekabidhiwa kwa Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani ambapo utembelea na kuzindua miradi mbali mbali ya maendeleo.

Akipokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge alisema kwamba katika mbio hizo mwenge huo utatembelea jumla ya miradi ipatayo 126.


Kunenge alibainisha kwamba mbio za Mwenge huo wa uhuru kwa mwaka huu  utakimbizwa katika Halmashauri tisa zilizopo katika Wilaya saba  ambapo jumla ya kilometa 1,225.3 zitakimbizwa katika maeneo mbali mbali.

Kunenge alifafanua kwamba kati ya miradi hiyo miradi 18 itawekewa mawe ya msingi,miradi 22 itazinduliwa na miradi ipatayo 86 itakaguliwa.

Aidha Kunenge alisema kuwa miradi hiyo itagharimu  kiasi cha shilingi Trilioni 8.536  ambapo serikali kuu imechangia bilioni 13.6,Halmashauri za wilaya shilingi bilioni 2.3 nguvu za wananchi na wawekezaji trilioni 8.5 na wadau wa maendeleo bilioni 14.6.

Pia alimshukuru Rais wa awamu ya sita kwa kuweka mazingira bora kwa ustawi na ufanisi zaidi katika sekta binafsi nchini.


Pia Kunenge katika hatua nyingine alisema kwamba katika kupambana na janga la ukimwi wameendelea kupambana kwa kutoa elimu ya upimaji wa wenza.

Kadhalika aliongeza katika kupambana na dawa za kulevya wameendelea kuimarisha mapambano kwa kubadilisha fikra,hisia na tabia.

Awali kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Godfrey Mnzava alizitaka halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaandaa nyaraka zote za miradi ya maendeleo.8

Saturday, April 27, 2024

DOZI MOJA INATOSHA KUFANIKISHA KUZUIA SARATANI SHINGO YA KIZAZI.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.

NI maadhimisho ya ‘dozi ya chanjo ya HPV’, inayomkinga mtoto wa kike asipate ugonjwa wa saratani ya mlango wa shingo ya uzazi.

Chanjo hiyo ya HPV inawalenga watoto wenye umri kati ya miaka tisa na 14, ambayo Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, anasema kuwa dozi moja inatosha kumkinga msichana kupata ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi. 

Waziri Ummy anayaongea hayo kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Dozi moja ya chanjo ya HPV kwa wasichana, akinena ni jukumu la wazazi na walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto kupata chanjo hiyo. 

Ni hafla iliyofanyika katika Viwanja vya Furahisha Wilayani Ilemela, Mwanza akiwa na ufafanuzi: “Wataalamu wetu ambao wanatoka kwenye Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). 

“Wametuhakikishia kuwa dozi moja ya chanjo ya HPV inatosha kumkinga msichana kupata saratani ya mlango wa kizazi.” 

Anasema awali dozi zilitolewa mbili, ya pili ikiwa ni miezi sita akipelekewa binti, hata hivyo wengi hawakurudi kumalizia. 

Lakini anaeleza mbadala uliopo ni kwamba, hivi sasa anasema wanatoa dozi moja, inayotosha kuwakinga wasichana dhidi ya maambukizi ya saratani ya mlango wa kizazi.  

Waziri anaeleza saratani inayoongoza kuwatesa Watanzania ni ‘Mlango wa Kizazi’ anayosema katika kila wagonjwa100, wako 23 wagonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.  

Anaorodhesha saratani zinazofuatia kwa ukubwa ni inayohusu: Mfumo wa Chakula, asilimia 11; matiti asilimia 10.4; tezi dume asilimia 8.9. 

Pia, Waziri anatoa wito kwa wazazi na walezi nchini, kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo zote wanazopaswa, ili wanufaike na kinga dhidi ya maradhi yaliyotajwa, ikiwamo lengo kubwa la kuwakinga na magonjwa, yakiwamo haya ya saratani pamoja na kuwakinga na vifo vinavyoweza kuzuilika na chanjo.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi.

  

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza, Saidi Mtanda atahakikisha watoto wote wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi 14, wanapata chanjo hiyo ili kufikia malengo.  

“Kwa mwaka 2022/23 Mkoa wa Mwanza ulifanikiwa kuchanja watoto zaidi ya laki Mbili sawa na asilimia 107 kati ya walengwa waliotarajiwa kuchanjwa ni laki 191,440 wenye umri chini ya mwaka mmoja, tumefikia malengo na kuyavuka,” anasema. 

Mkazi wa Jiji la Mwanza Amina Said, anasema kutolewa kwa chanjo hiyo ni moja ya mapambano ya kumkinga mtoto wa kike asipate saratani ya mlango wa kizazi. 

Anasema elimu juu ya chanjo hiyo inatakiwa kutolewa mara kwa mara ili jamii iendelee kuelewa umuhimu wa chanjo hiyo. 

"Mimi nina mtoto wa kike ana umri wa miaka name,lakini sina  elimu yoyote, kuwa anapofikisha miaka tisa anatakiwa kupatiwa chanjo hiyo," anasema. 

Anaongeza kuwa, serikali inapambana kuwahakikishia wananchi wake wawe na afya njema, hivyo ana rai elimu iendelee kutolewa kwa jamii, ijue umuhimu wa chanjo. 

Aziza Jumanne, mkazi wa Mwanza anaitaja chanjo hiyo kuwa mkombozi kwa wasichana wenye sifa ya kupata chanjo hiyo, akiishauri jamii izingatie jinsi ya kuwasaidia watoto wa kike wasipate ugonjwa huo. 

"Kila mzazi ambaye ana mtoto wa kike aliye na sifa za kupata chanjo, awapeleke kupata chanjo hiyo," anasema, kuwa watoto wanapopatiwa chanjo, wananudhurika kwa maradhi hayo.

 Anthony Andrew, mkazi wa Maduka Tisa, jijini Mwanza anasema ni wakati wa wazazi na walezi kuachana na mila potofu dhidi ya kuwapo chanjo hizo na kinachotakiwa ni kuisaidia serikali, ili watoto wapate waelewe.

 Andrew anakumbusha chanjo inatolewa bure na inabaki  jukumu la walezi na wazazi kujitokeza na watoto wao waweze kupatiwa chanjo hiyo. 

"Tumekuwa tunasikia kutoka kwa wataalamu wetu wa afya, magonjwa sugu yanayo changia vifo kwa jamii. Katika magonjwa hayo, saratani nayo ipo," anasema, akiwa na ufafanuzi.

 Anaongeza kuwa, saratani zote zina changamoto zake, kama mtu atachelewa kupata matibabu kwa wakati anayonafasi kubwa ya kupoteza maisha.













Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya waandishi wa habari wakichukuwa matukio na taarifa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV,  viwanja vya Furahisha Mwanza.
Binti aliyetia fora katika uwasilishaji wa shairi lenye kutia hamasa kwa wazazi kushiriki vyema kuhakikisha watoto wanapatiwa chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi, wakiwa katika Uzinduzi wa maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Sehemu ya baadhi ya wanafunzi wa shule mbalimbali za Jiji la Mwanza, wakiwa katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, katika viwanja vya Furahisha.
Kutoka Bujora ni kundi la ngoma likinogesha shughuli katika maadhimisho ya chanjo ya HPV, viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
 

Wednesday, April 24, 2024

MSIFANYE KAMPENI KINYEMELA KABLA YA MUDA WAKE -KATIBU CCM KIBAHA MJI


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Issack Kalleiya amekemea vikali tabia ya baadhi ya wanachama kuanza kufanya kampeni za chini chini na kutangaza nia kwa ajili ya kuwania nafasi mbali mbali za uongozi kabla ya muda kitu ambacho ni kinyume kabisa na taratibu za chama.

Katibu huyo ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi kata ya kongowe yenye lengo la kuweza kuzungumza na wanachama wa CCM ikiwa pamoja na kuimarisha uhai wa chama kuanzia ngazi za matawi,mashina pamoja na Kata husika.

Kalleiya ambaye katika ziara yake aliambatana na viongozi mbali mbali wa chama alisema kuwa lengo kubwa ni kuweka misingi imara ya kukijenga chama kuanzia katika ngazi za chini hadi ngazi za juu.

Aliongeza kuwa anashangazwa kuona baadhi ya wanachama kwenda kinyume na taratibu zilizowekwa kwa kuanza kutangaza nia kinyemela ya kuwania katika nafasi mbali mbali za uongozi.
"Nipo katika ziara yangu yemye lengo la kuona namna ya kusimamia mwenendo mzima kwa wanachama ili waweze kuimarisha uhai mzuri kuanzia katika ngazi za matawi,mashina na ngazi nyingine,"

"Kitu kingine ambacho nakemea vikali ni hili suala la baadhi ya wanachama kuanza kufanya kampeni za chini chini za kutaka kuwania nafasi mbali mbali za chama kwa kweli hii sio sahii kwani muda wake ni bado,"alisisitiza Katibu Kalleiya.

Aliongeza katika chama cha mapinduzi kuna miongozo ambayo ipo wazi katika mambo ya uchaguzi hivyo ni lazima kila mwanachama anapaswa kuwaacha viongozi waliopo madarakani wamalize muda wao bila kuvunjiwa heshima.

Katibu huyo pia alliwahimiza wanachama wote wa ccm kuhakikisha kwamba wanajisajili kwa mfumo mpya wa njia ua kieletroniki ili waweze kutambulika kwa urahisi.

Alisema kwamba kwa sasa chama kinaendelea kuwahimiza wanachama wake kufanya uchaguzi mbali mbali ili kuweza kujaza nafasi nafasi ambazo bado zimeachwa wazi.
Katika aliongeza kuwa chama cha mapinduzi kikiimarisha kuanzia katika ngazi za chini kitaweza kuleta matokeo chanya na kuibuka na ushindi katika uchaguzi  wa serikali za 
 mitaa ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu pamoja na uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Saturday, April 20, 2024

LEO BARABARA ZOTE ZA JIJI LA DAR ES SA;AAM KUELEKEA MWENGE - TANGAZO ANOINTED MINISTRY 2024

 𝗘𝘄𝗲 𝗺𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗠𝘂𝗻𝗴𝘂 𝗵𝗶𝗶 𝗶𝗻𝗮𝗸𝘂𝗵𝘂𝘀𝘂 𝗻𝗶 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝘁𝗮𝗿𝗲𝗵𝗲 𝟮𝟬𝘁𝗵 𝗔𝗽𝗿𝗶𝗹 𝟮𝟬𝟮𝟰 𝗗𝗮𝗿 𝗲𝘀 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺 𝗶𝘁𝗮𝘁𝗶𝗸𝗶𝘀𝗶𝗸𝗮....

. . . . . #JEMBEGOSPLE

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI PWANI LAWAFUNDA WANANCHI JUU YA KUJIKINGA NA MAFURIKO NA MAAFA

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Katika kukabiliana na majanga mbali mbali yakiwemo ya  moto na mafuriko ya mvua imetoa elimu kwa zaidi ya wananchi 72862 juu ya kujikinga na majanga pindi yanapotokea.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima wakati akizungumzia mipango na mikakati waliyojiwekea katika kupambana na majanga ya aina tofauti.

Kamanda Shirima alisema kwamba lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi juu  ya kujikinga na majanga mbali mbali hasa katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

"Sisi kama jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani tumeendelea kutoa elimu kwa wananchi wetu na kwamba tumeshafanikiwa kwa kuwafikia wananchi wapatao 72862 na kimsingi bado tunaendelea,"

"Katika zoezi ili la kutoa elimu kwa wananchi wetu wa Mkoa wa Pwani tangu Julai 2023 hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu tumepiga hatua kubwa ya kutoa elimu hiyo ambayo idadi yake ni 72862,"alisema Kamanda Shirima.

Kadhika Shirima alifafanua kuwa pamoja na kutoa elimu hiyo pia wameweza kupata fursa ya kutoa elimu juu ya tahadhari dhidi ya mafuriko ambayo yanatokea kutokana na mvua.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alibainisha kuwa wameshapita kutoa elimu katika mikusanyiko ya watu mbali mbali ikiwa sambamba na kuanzisha sehemu maalumu za Fire club ambazo zitasaidia katika kupambana na majanga.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo aliwasisitiza wananchi ambao wamefanikiwa kupatiwa mafunzo hayo kuendelea kuyatumia vizuri ili yaweze kuwa msaada mkubwa katika jamii inayowazunguka.

Friday, April 19, 2024

RFO PWANI-TUMEFANIKIWA KUOKOA WANANCHI 2397 MAFURIKO YA RUFIJI NA KIBITI

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima amesema kwamba hadi kufikia leo Aprili 19 wamefanikiwa kuokoa wananchi wapatao 2397 kutoka Wilaya za Rufiji na Kibiti mkoani Pwani ambao walikubwa na mafuriko ya mvua na makazi yao kuzingirwa na maji.

Akizungumza katika mahojiano maalumu kuhusiana na mwenendo mzima wa hali halisi ilivyo kwa sasa  Kamanda huyo alibainisha hali ya makambi ambayo yametengwa kwa ajili ya wahanga yapo salama.






Kamanda huyo alisema kwamba kutokana na mvua ambazo zinaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali ziliweza kusababisha baadhi ya wananchi kukosa  makazi yao na hivyo serikali kuamua kuwatafutia maeneo mengine ambayo ni salama zaidi.

Alisema kwamba wameweza kufanikisha zoezi la uokoaji wa wananchi hao kwa kushirikiana bega kwa bega na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa lengo la kuwatoa wananchi katika maeneo yaliyozingirwa na maji.

"Kwa sasa wananchi wote ambao tumeweza kufanikiwa kuwaokoa wameifadhiwa na serikali katika makambi maalumu ambayo yapo katika Wilaya ya Rufiji na Kibiti na yapo katika hali salama ", alisema Kamanda Shirima.

Kadhalika alibainisha kuwa tangu zoezi hilo lilipoanza mnano tarehe 9 machi mwaka huu la kuwavusha watu katika maeneo mbali mbali ambayo wanayooshi ili kuwapeleka maeneo salama.

Pia aliongeza kuwa zoezi rasmi kwa ajili ya uokoaji wa watu ambao wanaishi katika maeneo mengine ya mbali lilianza kufanyika kuanzia Aprili 7 mwaka huu hadi kufikia leo hii kufikia idadi ya watu waliookolewa kufikia 2397.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alitoa rai kwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti pamoja na Rufiji kuhakikisha wanaondoka katika maeneo hatarishi na kukubali kwenda katika maeneo salama ambayo yametengwa na serikali.

Nao baadhi ya wananchi wa   Wilaya ya Kibiti na Rufiji wameishukuru kwa dhati serikali pamoja na wadau mbali mbali wa maendeleo kwa kuwapatia misaada ya kibinadamu kutokana na kupata mafuriko hayo.

Pia hawakusita kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani kwa kujituma kwa kipindi chote katika kuwasaidia na  kuokoa maisha yao.

WAZIRI JERRY SILAA KUONGOZA KLINIKI YA ARDHI TANGA

 

Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.

Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.

“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema

Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.

Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani

Thursday, April 18, 2024

RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA ALAT 2024 UTAKAOFANYIKA ZANZIBAR

 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 mgeni rasmi Mkutano wa 38 ALAT utakaofanyika Tarehe 23 - 25 April 2024 #Zanzibar

. . #alat @ortamisemi @samia_suluhu_hassan @dr.hmwinyi @jembenijembe @kikotifredy #samiasuluhuhassan #HUSSEINMWINYI #zanzibar